Thursday 10 July 2014

Hajj imetajwa katika Quran na Biblia

Wengi hawakujua kwamba Ibada ya Hajj imetajwa hata katika Biblia ...

Kwanza kabisa, tunajua kwamba moja ya jina la "Makkah" ni "Baka" kama ilivyotajwa katika Qur'an (3:96)



Hakika Nyumba ya kwanza walio wekewa watu kwa ibada ni ile iliyoko Baka (Makkah), iliyo barikiwa na yenye uwongofu kwa walimwengu wote. (Quran 3:96)


Biblia (Zaburi) inasema,

{84:3} Hata shomoro wamepata makao yao,
mbayuwayu wamejenga viota vyao,
humo wameweka makinda yao,
katika madhabahu zako, ee Mwenyezi-Mungu wa majeshi,
Mfalme wangu na Mungu wangu!

{84:4} Heri wale wanaokaa nyumbani mwako,
wakiimba daima sifa zako.

{84:5} Heri watu wanaopata nguvu zao kwako,
wanaotamani kwenda kuhiji mlimani kwako.

{84:6} Wapitapo katika bonde kavu la Baka,
hulifanya kuwa mahali pa chemchemi,
na mvua za vuli hulijaza madimbwi.

{84:7} Wanaendelea kupata nguvu zaidi na zaidi;
watamwona Mungu wa miungu huko Siyoni.

{84:8} Usikie sala yangu ee Mwenyezi-Mungu wa majeshi;
unitegee sikio, ee Mungu wa Yakobo.

{84:9} Ee Mungu, umwangalie kwa wema ngao yetu mfalme,
umtazame huyo uliyemweka wakfu kwa mafuta.

{84:10} Siku moja tu katika maskani yako,
ni bora kuliko siku elfu mahali pengine;
afadhali kusimama mlangoni pa nyumba yako,
kuliko kuishi nyumbani kwa watu waovu.

{84:11} Mwenyezi-Mungu ni jua letu na ngao yetu;
yeye hutuneemesha na kutujalia fahari.
Hawanyimi chochote kilicho chema,
wale waishio kwa unyofu.

{84:12} Ee Mwenyezi-Mungu wa majeshi,
heri mtu yule anayekutumainia wewe!

wakati Waislamu wana Hiji wao huimba (kumtukuza Mungu) hivi "Labaik allahumma labaik, labaikellah sharika lakalla baik, innal hamda wanneeamata laka wa mulk " (Sisi tupo hapa katika huduma yako ee Mola, Sisi tupo hapa katika huduma yako na Wewe huna washirika. zako peke yako ni Sifa zote na zote fadhila, na yako peke yako Mamlaka. Wewe huna washirika).

Mtume Mohammed saw kasema kwamba:

"Sala moja hapo katika Maskani ya Mwenyezi Mungu (Baka) ni bora kuliko sala elfu mahali pengine."

Hata chemchemi ya zamzam iliopo Baka (Makkah) imetajwa katika Aya hizo za Biblia. 

Hapo Baka haramu kuinda (hata ndege), pia tunaona aya za Biblia pia zinasema kwamba hapo Baka Hata shomoro wamepata makao yao, mbayuwayu wamejenga viota vyao,
humo wameweka makinda yao... 

Aya hizi za Biblia kutoka; Biblia Habari Njema (BHN)

Unaweza kuipata Biblia hiyo online katika link hii hapa chini

https://www.bible.com/en-GB/bible/74/psa.84.3.bhn


2 comments: