Thursday 10 July 2014

Wapendwa someni haya bila hasira kisha amueni wenyewe kama ni sahihi au sio sahihi

Salamu na amani iwe juu ya mwenyekufuata uongofu.

Wapendwa,

Tafadhali someni aya hizi kisha tafakarini,


Biblia inasema ...wakufahamu wewe ambaye pekee ni Mungu wa kweli,nakumfahamu Yesu Kristo ambaye umemtuma. (Yohana17:3)

Hapa tunaona kwamba Yesu katumwa na Mungu wa Pekee.

Huyu ndio Mungu (Mungu Mmoja tu), soma aya hizi,;

Biblia inasema , Yeye peke yake anaishi milele katika mwanga usioweza kukaribiwa na mtu. Hakuna mtu aliyepata kumwona au awezaye kumwona. Kwake iwe heshima na uwezo wa milele! Amina. (1 Timotheo 6:16)

Quran Inasema, Macho hayamfikilii bali Yeye anayafikilia macho. Naye ni Mjuzi, Mwenye khabari. (Quran 6:103)

Quran Inasema, Mwenyezi Mungu, hakuna mungu ila Yeye Aliye Hai, Msimamizi wa yote milele. (Quran 3:2)

Quran Inasema, Yeye ndiye anaye kuundeni ndani ya matumbo ya wazazi kwa namna apendayo. Hapana mungu ila Yeye, Mwenye nguvu na Mwenye hikima. (Quran 3:6)

Quran Inasema, Mwenyezi Mungu, na Malaika, na wenye ilimu, wameshuhudia kuwa hakika hapana mungu ila Yeye, ndiye Mwenye kusimamisha uadilifu; hapana mungu ila Yeye Mwenye nguvu na Mwenye hikima. ( Quran 3:18 )

Quran inasema, Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Njooni kwenye neno lilio sawa baina yetu na nyinyi: Ya kwamba tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu, wala tusimshirikishe na chochote; wala tusifanyane sisi kwa sisi kuwa Mabwana badala ya Mwenyezi Mungu. Na wakigeuka basi semeni: Shuhudi- eni ya kwamba sisi ni Waislamu. (Quran 3:64)

No comments:

Post a Comment