Thursday 10 July 2014

Mkristo ananiambia....

Kitu cha kushangaza kabisa kuona Mkristo ananiambia ati mwamini Yesu yaani Nabii Issa A.S.. Hajui kuwa Nabii Issa katajwa ndani ya kitabu cha Mwenyezi Mungu Qur-ani. Lakini hata hivyo anataka nimwamini vipi?

Mtume au Mungu au Mtoto wa Mungu? Ikiwa nimwamini kuwa Mtume wa Mungu, basi Waislamu wamekwisha mwamini toka miaka 1400 iliyopita ilipoteremshwa Qur-ani.

Mzungu alikwenda kwa bushman kisha akamwabia mwamini Yesu kuwa ni Mungu. Bushman alimuuliza swali moja tu. Jee, huyu Mungu unayetaka nimwamini anakula?

Mzungu akamjibu kuwa anakula. Kwahiyo bushman akamwambia ikiwa anakula basi anakwenda chooni. Kwahiyo hafai kuwa Mungu huyo ni binadamu kama mimi wala simwamini.

Ingelikuwa Mola hakutufunulia kuhusu Yesu/Nabii Issa A.S.katika kitabu chake bila shaka tungewaamini wakristo wasemavyo. Lakini tunamshukuru Mola kateremsha Sura kamili ya mama yake Yesu aitwaye Mariam/Mary.

Na katuelezea jinsi alivyoshika mimba au ujauzito mpaka kumzaa Nabii Issa. Na vipi aseme wakati watu watakapomuuliza amempata wapi mtoto na hali hakuolewa?

Na kwanini Mola akateremsha Surat Mariam kamili ya mama yake Yesu/Nabii Issa lakini hakutajwa mama yake Mtume Muhammad S.A.W.. Kwasababu Mtume S.A.W. hakuzaliwa kimiujiza kama alivyozaliwa Nabii Issa na wala hapakuwa na tatizo la watu kumuabudu kama walivyomuuitakidi Nabii Issa kuwa ni Mungu au Mtoto wa Mungu.

No comments:

Post a Comment